Alhamisi, 23 Juni 2016

VARDY AONGEZA MKATABA LEICESTER CITY.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa
wa England, Jamie Vardy
amekubali kusaini Mkataba
mpya wa miaka minne
kuendelea kuchezea klabu
yake, Leicester City na
kukataa ofa ya kujiunga na
Arsenal.
Mustakabali wa mkali huyo
wa mabao wa England
umekuwa haueleweki tangu
Arsene Wenger atangaze ofa
ya Pauni Milioni 20
kumnunua Juni 3, mwaka
huu, lakini ameipiga chini ofa
hiyo na kuamua kubaki
Uwanja wa King Power.
Baada ya Arsenal kumpa ya
mshahara wa Pauni 120,000
kwa wiki, Leicester City nayo
imemuongezea mshahara
mchezaji huyo hadi pauni
100,000 kwa wiki na Vardy
atasaini Mkataba mpya
atakaporejea kutoka kwenye
Euro 2016 nchini Ufaransa.
Vardy aliisaidia Leicester City
kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu
ya England akifunga jumla ya
mabao 24 msimu uliopita
Mbali ya mshahara mkubwa
zaidi, lakini Vardy
angenufaika zaidi kwa kipato
Uwanja wa Emirates kutokana
na hali nzuri ya kiuchumi na
sera za malipo za Arsenal
ukilinganisha na Leicester.
Iwapo atasaini Mkataba
mpya, mchezaji huyo
mwenye umri wa miaka 29
atadumu King Power hadi
mwaka 2020 atakapofikisha
umri wa miaka 33 – jambo
ambalo ni habari njema kwa
kila mmoja ndani ya
Leicester City.
Vardy alikuwa chachu ya
mafanikio ya Leicester City
msimu uliopita ikitwaa
ubingwa wa Ligi Kuu ya
England, akifunga jumla ya
mabao 24.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni