Meneja wa Manchester City Pep Guardiola anaamini ameshinda mbio za kumsajili beki wa Everton John Stones, 22, lakini Chelsea na Manchester United bado pia wanamfuatilia (Sun), Kiungo wa Spain na Chelsea Cesc Fabregas, 29, anasema uamuzi wa Uingereza kujiondoa kutoka Umoja wa Ulaya utaathiri Ligi Kuu ya England (Sunday Telegraph), meneja wa Arsenal Arsene Wenger anatarajia kukutana na wawakilishi wa mshambuliaji wa Lyn, Alexandre Lacazette, 25, lakini anakabiliwa na ushindani kutoka Atletico Madrid na West Ham (Sunday Mirror), meneja wa Manchester United Jose Mourinho anaghadhibishwa na mkakati wa usajili wa Old Trafford kwa kumsajili beki mmoja tu Eric Bailly, 22, mpaka sasa (Manchester Evening News), Manchester United watalazimika kuvunja rekodi ya dunia ya pauni milioni 85.3 ambayo Real Madrid walitoa kumsajili Gareth Bale, ikiwa wanataka kumsajili kiungo wa Juventus Paul Pogba, 23 (Sunday Telegraph), Jose Mourinho ana uhakika kuwa pauni milioni 30 zitatosha kumsajili winga wa Wolfsburg Julian Draxler, 22, ikiwa atashindwa kumpata Henrikh Mhkitaryan, 27 kutoka Borussia Dortmund (Star on Sunday), Tottenham wanakabiliwa na ushindani kutoka Paris St-Germain kumsajili mshambuliaji wa AZ Almaar Vinvest Janssen, 22 (L’Equipe), Bayern Munich wamevutiwa na uchezaji wa kiungo wa Tottenham Eric Dier, 22, kwenye michuano ya Euro 2016 (Sunday People), meneja mpya wa Everton Ronald Koeman anataka kumsajili kiungo wa Manchester United Morgan Schneiderlin, 26 (Sunday Mirror), Stoke watakamilisha usajili wa mshambuliaji wa West Brom Saido Berahino, 22 wiki hii (Sunday People), Swansea wanakaribia kumsajili beki wa kari wa Ajax Mike van der Hoorn, 23, kwa mkataba wa pauni milioni 2 (Mail on Sunday), meneja wa Newcastle Rafael Benitez anajiandaa kutoa dau la pauni milioni 10 kumsajili kiungo wa Bournemouth Matt Ritchie, 26, kutokana na wasiwasi kuwa huenda Andros Townsend, 24, anaweza kuondoka (Sun).

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni