Alhamisi, 23 Juni 2016

SALUM KIMENYA ATAKA MIONI 40 KUMWAGA WINO MSIMBAZI

Beki wa kati wa Tanzania Prisons, Salum Kimenya,
amesema anahitaji Sh milioni 40 ili aweze
kumwaga wino kwenye kikosi cha Wekundu wa
Msimbazi, Simba, kwa mujibu wa Mtanzania.
Kimenya ambaye amekuwa kwenye kipindi cha
mafanikio msimu uliopita, amesema hakuna
kinachomkwamisha kutua kwenye klabu hiyo zaidi
ya fedha anayoitaka.
Alisema dau dogo ambalo amekuwa akitajiwa na
viongozi hao wa Simba, ndilo limekuwa kikwazo
cha yeye kutua kwenye klabu hiyo.
“Simba mwaka jana walinitaka wakataka kunipa
milioni 30 nikakataa nikawaambia nipeni 45 dili
likavunjika na safari hii nawashangaa kabisa dau
lao eti wanataka kunipa Sh milioni 20,
nimewaambia wanipe 50 pia imekuwa ni kuomba
wapunguziwe sasa imefika 40 hapo siwezi
kupunguza tena,” alisema.
Kimenya alisema amewapa muda viongozi hao wa
Simba mwisho wiki hii, ikifika Jumatatu ijayo basi
atatia saini kwenye klabu yake ya Prisons.
“Nawapa mpaka wiki hii iwe mwisho kama
wakikaa kimya basi nitasajili kwenye klabu yangu
ya Prisons ambayo nimemaliza nayo mkataba,”
alisema.
Simba inasuka upya kikosi chake msimu ujao
ambapo mpaka sasa tayari imewasajili nyota
watano ambao ni mabeki; Emmanuel Semwanza,
kiungo Muzamil Yasir, Mohammed Ibrahim, Hamad
Juma na mshambuliaji, Jamal Mnyate.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni